Psalms 2:1-6

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu


1 aKwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,
na kabila za watu kula njama bure?

2 b cWafalme wa dunia wanajipanga
na watawala wanajikusanya pamoja
dhidi ya Bwana
na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

3 dWanasema, “Tuvunje minyororo yao
na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”


4 eYeye atawalaye mbinguni hucheka,
Bwana huwadharau.

5 fKisha huwakemea katika hasira yake
na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

6 g“Nimemtawaza Mfalme wangu
juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Copyright information for SwhKC